ULEGA AMSIMAMISHA KAZI AFISA MFAWIDHI KIGOMA

  


Na Mwandishi wetu,Kigoma

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega amemuagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Agnes Meena kumsimamisha kazi Afisa Mfawidhi anayeshughulikia ubora wa samaki kituo cha Kigoma,Frank Kabitina kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma.

Waziri Ulega ametoa maelekezo hayo alipokuwa akizungumza na wananchi katika Mwalo wa Katonga Mkoani Kigoma Januari 9, 2024.

Amesema Afisa huyo amekuwa akikusanya mapato ya mazao ya uvuvi na sehemu ya mapato hayo akiyatumia kwa manufaa yake binafsi.

“Naibu Katibu Mkuu, Afisa huyu hakuna haja ya kusema achunguzwe, mtoe kwanza wakati mtakapokuwa mnaendelea kumchunguza na atakayekuja mtahadharisheni, tunataka mtu muadilifu”, amesema

Powered by Blogger.