HIFADHI YA BURIGI CHATO TAYARI KUPOKEA WATALII

***yatumia  sh 3.3 bilioni kukarabati Miundombinu ya hifadhi 

Na Mwandishi wetu 

Hifadhi ya Taifa ya Burigi -Chato imetumia kiasi cha sh bilioni  3.3 kuimarisha Miundombinu ndani ya hifadhi ili kuvutia watalii kutembelea hifadhi hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 2019.

Akizungumza na waandishi wa habari,Mkuu wa hifadhi hiyo, Kamishina Msaidizi Ismaili Omari alisema Maboresho ya Miundombinu ya hifadhi ni  jitihada zinazofanywa na Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA )kuboresha miundo mbinu  mbalimbali ndani ya hifadhi hiyo kufikia  malengo ya serikali Tanzania kupokea milioni 5 ifikapo mwaka 2025

Mhifadhi Omar amesema barabara zenye urefu wa kilomita 97.5 pamoja na madaraja na vivuko yamejengwa hadi sasa umekamilika ujenzi wa kambi za Utalii pamoja na  makazi ya bei nafuu ya watalii ndani ya hifadhi hiyo.

"Tumejenga barabara zinapitika wakati wote lakini pia madaraja na kuna minara ya Mawasiliano ambayo imejengwa ndani ya hifadhi  tofauti na miaka ya nyuma,hivi sasa Watalii wanaweza kuwasilisha"amesema

Afisa utalii hifadhi ya Burigi- Chato ,Aldo Mduge amesema upekee wa hifadhi hiyo ni uwepo wa ndege aina ya Domo kiatu (African Shoebill) maziwa yanayo zunguka hifadhi  wanyama wengi na ndege aina 400.

Akizungumzia makazi ya ndani ya hifadhi, Kaimu mkuu idara ya utalii hifadhi  hiyo, Emmanuel Nyundo hiyo alisema uwekezaji walio ufanya ikiwemo kujenga kambi ya wageni ya kudumu huku  akiwakaribisha   wageni kuwekeza Burigi kwani kuna maeneo mazuri.

Hifadhi hii  ina kilomita za mraba 4707 katika wilaya za Biharamulo,Chato,Karagwe ,Ngara na Muleba,ipo katika mikoa ya Kagera na Geita.


Powered by Blogger.