Kiungo wa Young Africans, Mudathir Yahya, amepewa adhabu ya kutocheza mechi tatu na pia atawajibika kulipa faini ya Tsh 1,000,000 kwa kumpiga kwa kiwiko Ibrahim Abraham wa Pamba Jiji FC wakati wa mechi yao kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.
Atakosa mechi ya derby dhidi ya Simba SC.