CHELSEA YAMTUPIA VIRAGO KOCHA WAKE BAADA YAKUPOKEA VIPIGO VITANO MFULULIZO
𝘽𝙍𝙀𝘼𝙆𝙄𝙉𝙂 𝙉𝙀𝙒𝙎: Klabu ya Chelsea imethibitisha kuachana na aliyekuwa kocha mkuu wa klabu hiyo, Liam Rosenior baada ya kuhudumu klabuni hapo kwa miezi minne tu hatua inayokuja kufuatia mwenendo usioridhisha wa klabu hiyo.
Rosenior 41, raia wa England ambaye alitua klabuni hapo mnamo Januari, 2026 akichukua mikoba ya Enzo Maresca ametupiwa virago baada ya klabu hiyo kupoteza mechi tano mfululizo za Ligi Kuu England bila kufunga bao lolote, rekodi ambayo haijashuhudiwa klabuni hapo tangu mwaka 1912.
Aidha Chelsea imemteua Calum McFarlane kuwa kocha mkuu wa muda wa klabu hiyo mpaka mwisho wa msimu huku klabu hiyo ikikabiliwa na jukumu la kumaliza nafasi tano za juu kwenye msimamo wa ligi kuu England ili kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.

