MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEKITI WA KAMATI YA TEIT


 

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Hamza Johari amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kamati ya Taasisi ya Uhamasishaji, Uwazi na Uwajibikaji Katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) , Balozi Wilson K. Masilingi, tarehe 14 Aprili, 2026 katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Bungeni,  Jijini Dodoma.

Balozi Masilingi ambaye aliteuliwa  na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya  TEITI Januari 29, 2026 amemtembelea Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kujitambulisha na kumpongeza  kwa kutekeleza kwa ufanisi majukumu ya kuishauri Serikali katika masuala ya kisheria Nchini.


Aidha, katika Kikao hicho, Viongozi hao wamejadiliana namna bora ya kuimarisha zaidi Ushirikiano uliopo baina ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na TEITI. 


 Katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya TEITI aliambatana na Katibu Mtendaji wa TEITI B

Mariam Mgaya.

Powered by Blogger.