EASTER AOMBA MSAADA KWA WATANZANIA




Na Mwandishi wetu, MOROGORO 

Mtoto Esther Daudi Athanas (9) mkazi wa Kijiji cha Ruhembe, Tarafa ya Mikumi Mkoani Morogoro, amelazimika kukaa nyumbani kwa muda wote  kutokana na kukosa msaada wa matibabu ya changamoto kutoa haja kubwa kupitia tumboni.

Mkaguzi Shayo amesema, Siku ya Mei 20, 2024  Easter akiwa anacheza na watoto wenzake mtaani alimuona Askari Polisi Shayo  Ambaye ni  Polisi  Kata wa  Kata ya  Ruhembe ghafla akakimbia  nyumbani kumwambia dada  yake kuwa anataka amfuate yule Askari  ili amuombe msaada wa  kupata matibabu ili  na yeye aweze kwenda Shule  kama  wenzake  kwa  kuwa  anatamani s ana kusoma kama ndugu zake.  Alimfuata Polisi  Kata na  kuanza kumlilia  machozi ili  amsaidie apate matibabu  ya  tatizo  alilonalo  na  baadae aweze kwenda  Shule . 

Kiu ya  Easter  ni  kutibiwa na  kwenda  Shule.

Polisi Kata wa Shayo ameendelea kusema kuwa  Esther wamezaliwa mapacha ambaye pacha mwenzake anasoma darasa la pili katika shule ya Msingi Kitete iliyopo Katani hapo.

“Katika familia yao nzima wapo watoto 6 ambapo wengine ni wakubwa zake, pacha wake Easter yupo darasa la pili shule ya msingi Kitete,”amesema Shayo

Mkaguzi Shayo ameendelea kusema kuwa Easter amezaliwa na tatizo la kupata haja kubwa kupitia ubavuni(tumboni) na si kwa njia ya kawaida.

“Tatizo hilo limesababisha yeye kushindwa kusoma shule kama pacha wake kwa kuwa amekuwa wa kufungwa vibwende na mama yake ili haja kubwa inapotoka izuiwe na vibwende hivyo,”amesema.

Amesema Mama yake Easter ni bubu ambaye hawezi kuzungumza ambapo baba yake aliondoka nyumban miaka mitatu iliyopita na kuwaacha wao na mama yao pekee.

“Mama yake Esther hana kazi yoyote zaidi ya kulima vibarua kwenye mashamba ya watu ili kupata chakula cha kujikimu yeye na watoto wake,”amesema.

Mawasiliano ya Mkaguzi Shayo -0675 325 388

Powered by Blogger.