MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI APEWA MAAGIZO NA BUNGE,SERIKALI

 



SPIKA wa Bunge Mussa Zungu amemtaka  Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Hamza Johari kuchukua   hatua kali dhidi ya Taasisi na Mashirika ambayo yalikaidi ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Utekelezaji wa Mikataba ya miradi mbalimbali kama ilivyoripotiwa na mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG 


Ameyasema hayo jana Aprili 1,2026 Bungeni Dodoma wakati wa hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika mwaka wa fedha 2026/27


Wakati huo huo Nae Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba amemuelekeza Mwanasheria huyo Mkuu kukaa pamoja na Wizara ya  Ardhi na TAMISEMI ili waandae mpango mkakati madhubuti katika kuhakikisha kwamba wanapata ufumbuzi wa kudumu juu ya migogoro ya ardhi inayoongezeka kila siku na kuwa kero  kwa Wananchi.

Powered by Blogger.